Johanna Konta Ameingia kwenye ratiba Hii nzito kulitafuta taji la Wimbledon

Mchezaji tennis namba moja nchini Uingereza, Johanna Konta amesema kuwa majira haya ya joto atakuwa na ratiba ngumu zaidi kuelekea michuano ya Wimbledon.



Konta ameyasema hayo kufuatia kuingia katika mashindano matatu kwa mpigo ambayo ni Nottingham Open, Birmingham Classic na Eastbourne International yatakayo muwezesha kuwafiti wakati wa michuano yaWimbledon.
 
Johanna Konta mwenye umri wa miaka 26, mwaka jana alishindwa kufanya vizuri katika michuano hiyo ya Nottingham Open hata hivyo alifanikiwa kuwa mwanadada wa kwanza wa Uingereza kufika hatua ya nusu fainali ya Wimbledon kwa mchezaji mmoja mmoja tangu alivyoweza kufanya hivyo Virginia Wade mwaka1979.

“Huu ni moja kati ya msimu niupendao na hakuna wa kuufananisha hasa mashindano yakiwa nyumbani ambapo kuna mashabiki, marafiki na familia ikiwa nyuma yako inakushabikia,”amesema Konta kupitia chombo cha habari cha Skysport.



Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment