Klabu ya Barcelona imewekwa katika wakati mgumu wa kufuzu katika hatua
ya fainali ya Kombe la Mfalme nchini Hispania kwa kupata ushindi
mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya wababe Valencia.
Katika mchezo wa marudiano Kunako dimba la Mestalla, Barcelona
watahitaji goli au kuzuia wasifungwe hata goli moja dhidi ya Valencia
ambao kwa msimu ni klabu ya pili ambayo imeruhusu magoli machache La
Liga.
Goli pekee la Barcelona limefungwa na Luis Suarez kunako dakika 67 ya mchezo.

0 comments :
Post a Comment