Bodi ya Ligi (TPLB) pamoja na
Shirikisho la Soka nchini (TFF) imesema inasubiri kamati ya saa 72 baada ya mechi za Ligi
daraja la kwanza FDL kukamilika ili kutangaza timu sita zilizopanda rasmi
kushiriki Ligi kuu msimu ujao.
Mtendaji mkuu wa bodi ya Ligi
Boniface Wambura amesema, ni kanuni ndizo zinazoelekeza kwamba ndani ya saa 72
baada ya mechi zote kumalizika timu zinanafasi ya kupeleka malalamiko yoyote
kama yapo.
"Kwahiyo sisi kikanuni
tutatangaza timu zilizopanda rasmi mara baada ya saa 72 kutimia, "
amesema.
Wambura amesema mpaka sasa
hawajapokea malalamiko yoyote kutoka kwenye timu za FDL hivyo wanaendelea
kusubiri kama kanuni inavyosema.
0 comments :
Post a Comment