KOMBE LA KRISMAS LAANZA KULINDIMA WILAYANI UKEREWE

 

Ligi maalumu ya sikukuu ya krismas imeanzishwa wilayani ukerewe mkoani Mwanza zikiwa ni jitihada za kuinua vipaji kwa vijana wilayani humo.

Michuano hiyo imeandaliwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji cha Victoria Youth Sport Academy(Viyosa)kwa udhamini wa Blog ya michezo inayoitwa Boiplus.

Kivumbi cha michuano hiyo kinafanyika katika uwanja wa Getruda Mongela mjini Nansio ikiwa imeanza 19/12 na tamati ni kwenye sikukuu za krismas tar 25/12/2016 ambapo siku hiyo pia ni maalumu kwaajili ya kukitambulisha kituo hicho cha michezo.

 

Katika mechi ya ufunguzi Viyosa fc imeibuka na ushindi kwa njia ya penati  6-5 baada ya dakika 90 za sare ya bao 2-2 dhidi ya timu ya Namagondo fc hivyo viyosa c imefuzu moja kwa moja kwenda nusu fainali.

Akizungumza na kipindi cha kona ya michezo cha 98.2 kwaneema fm radio mkurugenzi wa kituo cha Viyosa Abdulaziz Makongo maarufu kama mwalimu Dulah amesema kutokana na ligi hiyo kuchelewa kuanza wameona ni bora wakaendesha mashindano hayo kwa mfumo wa mtoano.

Mwalimu dulah amesema michuano hiyo inashirikisha timu nane zote za wilayani ukerewe kwa vijana wa umri chini ya miaka 17.

Timu zinazoshiriki katika michuano hiyo ni Viyosa fc,Namagondo fc,Kagera fc,Yoso fc,Udc fc,Nantare fc,Butiliti fc na Boma fm.

Zawadi zitakazotolewa kwa msindi wa kwanza ni Tsh150,00/= Mshindi wa pili ni Tsh100,000/= na Mshindi wa tatu ni Tsh50,000/=. Mfugaji bora atachukua Tsh25,000/=

Hapa chini tumekuwekea picha za mechi hiyo ya ufunguzi,karibu uzitazame:



                                         
Share on Google Plus

About Jacktan Msafiri

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment