Bwn: PETER OMARY ambaye ni mkurugenzi mpya wa kwa neema fm akiwa katika pozi.

Marium Juma Mtaalamu wa masoko akiwa na mkurugenzi
Program menegerJackline Raphael akiwa na mkurugenzi
Mtaalamu wa kipindi cha full shangwe extra Joshua Dede akiwa na
mkurugenzi
Chief Editor Jeston Kihwelo akiwa na mkurugenzi
Mtaalamu mwingine wa kipindi cha full shangwe extra Fabian Fanuel akiwa
na mkurugenzi
Mtalamu wa kipindi cha michezo Erasto Juma akiwa na mkurugenzi
Mwanahabari Dominic Felician akiwa na mkurugenzi
Uongozi wa kituo cha redio kwaneema
fm cha jijini mwanza umemtangaza
bwn:Peter Omary kuwa mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho ambaye atakuwa
mtendaji mkuu katika uendeshaji wa redio hiyo.
Bwn: Peter Omary anachukua nafasi
hiyo ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Askofu mkuu wa kanisa la TFE kwaneema
bishop Augastine Mpemba ambaye yuko nje ya nchi kimasomo kwa muda mrefu sasa.
Akizungumza muda mfupi baada ya
kutangazwa rasmi mbele ya wafanyakazi wa kituo hicho Bwn: Omary amesema
atahakikisha kituo hicho kinawanufaisha watanzania walio wengi kutokana na
mikakati mipya mbalimbali ilofikiwa ikiwa ni pamoja na kupitia upya vipindi vya
redio kwa lengo la kuviboresha zaidi.
Aidha Bwn: Omary amewataka
wasikilizaji wa 98.2 kwaneema fm radio kuendelea kukiunga mkono kituo hicho
likiwemo tamasha la miaka 5 tangu kuanzishwa kwake litakalofanyika JB Belmont
hotel 6/4/2015 kwa kuendelea kununua tiketi kwa wingi, ambapo pia amesema
hakuna kitakachobadilika bali ubora wa kituo kuongezeka kwa kasi siku hadi
siku.















0 comments :
Post a Comment