KIKOSI
cha Yanga kinaondoka leo mjini Mbeya kwenda Iringa tayari kwa mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Lipuli Uwanja
Samora Jumamosi wiki hii.
Yanga
inaondoka leo, ikiwa ni siku mbili tangu iwatoe wenyeji, Ihefu FC hatua
ya 32 Bora ya michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) kwa ushindi
wa penalti 4-3 baada ya sare ya 1-1 ndani ya dakika 90 Uwanja wa
Sokoine mjini Mbeya juzi.
Katika
mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, Ihefu ya Ligi Daraja la Pili
Tanzania Bara ilikaribia kuimaliza Yanga ndani ya dakika 90, kama si
bao la penalti la dakika ya mwisho la mshambuliaji Mzambia, Obrey
Chirwa.
Ihefu walitangulia kwa bao la kujifunga la beki wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’ dakika ya 36 katika juhudi za kuokoa shuti la Innocent Kapalata aliyepasiwa na Elias Salingo.
Baada ya bao hilo, Yanga waliokuwa wakicheza taratibu walikuwa kama waliopigwa mshituko na kuamka kwa kuongeza kasi ya mashambulizi.
Lakini safu ya ulinzi ya Ihefu ikiongozwa na kipa wake hodari, Andrew Kayuni iliwazuia watoto wa kocha Mzambia, George Lwandamina kupata bao.
Kipindi cha pili, Ihefu wakaamua kabisa kucheza kwa kujihami na huku wakipoteza muda kwa kujiangusha na kuchelewa kuanzisha mipira inapofuka upande wao.
Lakini Yanga waliendelea kuwa wastahmilifu huku pia wakibadili mbinu moja baada ya nyingine katika jitihada za kusaka bao la kusawazisha.
Hatimaye mpango wa kutafuta penalti wa Chirwa ukafanikiwa dakika ya kwanza ya muda wa nyongeza kati ya sita baada ya kutimia dakika 90 za kawaida za mchezo, pale Mzambia huyo alipoingia kwenye boksi na kwenda chini kwa urahisi baada ya kubanwa na mabeki wawili wa Ihefu.
0 comments :
Post a Comment