Maradona anyimwa visa ya kuingia Marekani kwa kumtusi Rais Trump.

Nyota wa zamani wa soka nchini Argentina Digo Maradona amenyimwa kibali cha kuingia nchini Marekani baada ya kudaiwa 'kumtusi' rais Donald Trump katika runinga.


Maradona alitarajiwa kusafiri kuelekea Miami kushiriki katika kusikilizwa kwa kesi ya mkewe wa zamani .

Lakini Maradona ambaye anasimamia klabu ya UAE ya Al Fujairah amekatazwa visa kwa mara nyengine kuingia Marekani. 

Katika mahojiano Maradona anadaiwa kumuita Trump 'Chirolita'.
Neno hilo ni tusi linalojulikana sana nchini Argentina likimaanisha watu ambao ni vikaragosi.

Wakili wa Mardona Matias Morla sasa atamwakilisha mtaja wake katika kesi hiyo mjini Miami.


Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment