ELIAS MAGULI AWEKA WAZI KILICHOMKAMISHA POLOKWANE CITY YA NCHINI AFRIKA KUSINI.

Akizungumza na Tiktaktz Maguli amesema, Mara baada ya kumalizika kwa michuano ya Cosafa mwezi Juni Mwaka jana nchini Africa kusini,   alisaini nao mkataba wa awali Mara baada ya kiridhishwa na kiwango chake lakini maslahi waliyokubaliana yalikiwa tofauti katika mkataba wa pili.

"Nilishasaini nao mkataba wa awali na tulikubaliana nilirudi kumalizana nao lakini katika awamu ya pili ilikuwa tofauti na ikumbukwe kipindi kile kilikuwa ni cha siasa Africa kusini na mwenyekiti wa Palokwane ni kiongozi wa siasa na ndiye mtoaji wa pesa kwahiyo nilipofika kulikuwa na mabadiliko kuhusu kiwango cha pesa tulichokubaliana ambapo kulikukuwa na mapungufu, "


Maguli amesema walijaribu kukaa na kuongea   ikiwa ni pamoja na kupiga hesabu ya pesa inayobakia na kuona bado haitoshi ukitoa kodi ambayo kwa mchezaji binafsi ni kubwa kwani mchezaji anatakiwa kujilipia kodi pamoja na kukodi gari suala ambalo walishindwana. 

Maguli amesema, aliamua kuondoka na kurudi Tanzania ambapo alikuta dirisha dogo la usajili limesogezwa mbele, na wakati bado yupo Tanzania Meneja wake alipigiwa simu kumtaka kurejea Afrika kusini ili asaini mkataba wa muda mfupi huku wakiangalia hali itakuwaje baada ya kumaliza mkataba huo ambapo uongozi wa Polokwane ulikataa na kumtaka asaini miaka mitatu kitu ambacho kilishindikana.

Kwa sasa Maguli bado yupo Tanzania na Meneja wake anaenndelea na taratibu za kumtafutia timu nyingine katika dirisha la usajili msimu ujao huku Maguli mwenyewe akisema yupo tayari kuichezea timu yoyote ya ndani au nje ya mipaka ya Tanzania iwapo wataafikiana kimaslahi.
Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment