<<<<<<<<VYUNGU VITATU VYA TIMU 11 KILA KIMOJA VYATAJWA!!
<<<<<<<<BONGO WAPO CHA 4 WAKIPITA RAUNDI YA AWALI!
Droo ya kupanga Makundi na Mechi za Raundi ya Awali itafanyika hapo Machi 10.
Mabingwa wapya wa Afrika, Nigeria,
pamoja na waliovuliwa Taji, Zambia, na Vigogo wengine wapo Chungu Namba 1
ikimaanisha Timu hizi haziwezi kuwekwa Kundi moja.
VYUNGU:
CHUNGU 1: Nigeria, Burkina Faso, Cote d’Ivoire, Togo, Mali, South Africa, Cape Verde, DR Congo, Zambia, Tunisia, Ghana.
CHUNGU 2: Egypt, Libya, Algeria, Senegal, Cameroon, Guinea, Sierra Leone, Gabon, Uganda, Congo, Central African Republic.
CHUNGU 3: Ethiopia, Benin, Angola, Niger, Zimbabwe, Equatorial, Mozambique, Malawi, Burundi, Liberia, Sudan.
CHUNGU 4: Timu 11 zitakazofuzu Raundi ya Awali
FAHAMU:
-Kundi litakuwa na Timu 4 na Makundi yatapangwa kwa kuchukua Timu moja toka kila Chungu.
-Hivyo, Timu za Chungu kimoja haziwezi kuwa Kundi moja.
Nchi ambazo zinatarajiwa kucheza Raundi
ya Awali kwa Mtindo wa Mtoano wa Nyumbani na Ugenini ni 21 na nazo ni
Tanzania, Botwsana, Chad, Kenya, Sao Tome & Principe, South Sudan,
Comoros, Lesotho, Madagascar, Mauritania, Somalia, CAR, Djibouti,
Eritrea, Gambia, Guinea Bissau, Mauritius, Namibia, Rwanda, Seychelles,
Swaziland.
Hii inamaanisha Mpinzania wa Tanzania katika Raundi ya Awali anaweza kuwa yeyote kati ya Timu 20.
0 comments :
Post a Comment