YANGA WAMEPIGWA MARUFUKU KUFANYA MAZOEZI UWANJA WA TAIFA.

Klabu ya Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wamezuiliwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa uliopo Jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi) asubuhi na kulazimika kuenda kufanya uwanja wa Polisi. 


Hayo amethibitisha na taarifa zilizotolewa na Afisa Habari wa timu hiyo Dismas Ten wakati alipokuwa anazungumza na mwandishi wa habari hii ya kutaka kujua sababu kubwa ya wao kuzuiliwa.

"Ni kweli tumezuiliwa kufanya mazoezi asubuhi ya leo kama nilivyotoa taarifa katika ukurasa wetu wa timu na meneja wa uwanja Nsajigwa Gordon ambapo ametuambia ule sio uwanja wa mazoezi ila upo kwa ajili ya mechi", amesema Dismas.

Timu ya Yanga inatarajia kushuka dimbani siku ya Jumamosi (Februari 10, 2018) kuvaana St. Louis inayotokea visiwa vya sheli sheli na katika mashindano ya kimataifa.


Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment