Liverpool inajiandaa kwa jaribio la
pili kumsajili kiungo wa wakti wa Monaco mwenye umri wa miaka 22 Thomas
Lemar wa Ufaransa baada ya kukataa kandarasi mpya katika klabu hiyo ya
ligi ya daraja la kwanza.
Mkufunzi wa Manchester City Pep
Guardiola hatoanzisha tena harakati za kutaka kumsajili winga wa
Leicester raia wa Algeria mwenye umri wa miaka 26 Riyad Mahrez mwishoni
mwa msimu huu. (mirror)
Mkufunzi wa zamani wa Barcelona Luis
Enrique ambaye anahusishwa na kuchukua mahala pake Antonio Conte wa
Chelsea anajiandaa kuelekea nchini Uingereza.
Hatahivyo mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 47 hataki kumrithi Conte hadi mwisho wa msimu huu.
Obrey Chirwa amempiku John Bocco katika harakati za kushinda
taji la mfungaji bora katika Ligi Kuu Bara, Lakini Okwi bado ndiye aliye
juu kwa mabao.
Chirwa aliyeanza wiki akiwa na mabao sawa na
mshambuliaji wa Simba alifunga hat-trick kaytika mchuano kati ya yanga
na Njombe mji katika uanwja wa kitaifa.
Tottenham inataka kumsaini kiungo wa kati wa Watford na Ufaransa Abdoulaye Doucoure mwishoni mwa msimu huu.
Beki
wa Brazil Fabinho mwenye umri wa miaka 24 ambaye klabu ya Manchester
United ilikuwa inamnyatia msimu uliopita anasema kuwa muda wake katika
klabu ya Monaco unakamilika(Metro)
Mshambuliaji wa Itali Fabio Borini na winga wa Uholanzi Jeremain Lens
wataondoka Sunderland mwisho wa msimu huu baada ya kubadilisha vifungu
vya sheria katika mkataba wao ambapo vinalazimu klabu zilizowasajili kwa
mkataba wa muda kuwanunua.
Wako katika mkopo katika klabu za AC Milan na Besikitas mtawalia. (Northern Echo)
Nottingham Forest inajiandaa kumsajili kipa wa Ugiriki Stefanos
Kapino. Mchezaji huyo mwnye umri wa miaka 23 aliondoka katika klabu ya
Olympiakos iliokuwa ikimilikiwa na mmiliki wa sasa wa klabu ya Forest
Angelos Marinakis baada ya migogoro kadhaa (Sun)
Mshambuliaji Benik Afobe, 24, atarudi katika klabu ya Wolvehampton
kwa kandarasi ya kudumu iwapo viongozi hao wa ligi ya daraja la kwanza
Uingereza watapandishwa katika ligi ya Premia.
Aliondoka katika
klabu ya Molineux ili kujiunga na Bournemouth mwezi Januari 2016 lakini
akarudi kwa mkopo mwezi Januari. (mirror)
Mshambuliaji wa Arsenal
Striker Pierre-Emerick Aubameyang, 28, anasema kuwa alijiunga na
Arsenal mwezi Januari baada ya kupigiwa simu na mchezaji wa zamani wa
Borussia Dortmund Henrikh Mkhitaryan. (Sky Sports)
Klabu za
K'Ogalo {Gor Mahia} na Ingwe{Leopard} nchini Kenya zina fursa nyengine
kuthibitisha thamani yao katika soka ya kimataifa barani Afrika wakati
watakapocheza nyumbani.
Mshambuliaji wa Ureno na Real Madrid Cristiano Ronaldo, 33, anasema
kuwa anaweza kuendelea kucheza kwa kipindi cha muda mrefu ujao.. (GQ -
in Italian)
Beki wa Manchester United Luke Shaw anatarajiwa kutia saini kandarasi mpya mwishoni mwa msimu huu.
Arsenal imeanza mazungumzo na kiungo wa kati Ainsley Maitland-Niles
kuhusu mkataba mpya. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kutolka
uingereza amesalia na miezi 18 mkataba wake kukamilika. (ESPN).






0 comments :
Post a Comment