IFAHAMU MIPANGO YA MANISPAA YA KINONDONI KWENYE MPIRA WA MIGUU NCHINI NIMEKUWEKEA HAPA.


Mara baada ya Timu ya KMC kufanikiwa kupanda daraja msimu huu kushiriki Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara msimu ujao wa 2018/19, Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjanin Sitta amesema kwa kushirikiana na uongozi wa Timu hiyo watahakikisha timu inakuwa mfano kwa taasisi nyingine kwa kukuza vipaji.


Sitta amesema, atahakikisha  wanakuwa na Shule ya kukuza vipaji kwa vijana ili  kupata wachezaji wazuri wa Klabu na timu ya Taifa ambao wataweza kuitangaza Tanzania kupitia Soka hapo baadaye.

Meya Sitta amesema, kwa sasa wanaendelea kuhakikisha waiboresha zaidi timu hiyo ambapo Siku ya Jumamosi ya Februari 10  wanatarajia kuwa na sherehe ya kukabidhi timu hiyo kwa wananchi ambao ndio wenye timu.

Meya Sitta ameongeza kuwa mbali na hayo, lakini kwa sasa yupo katika mazungumzo na wadau pamoja na wadhamini mbalimbali ili kuweza kupata watu watakaoweza kuibeba timu hiyo na kuweza kufanikisha malengo yao ya muda mrefu na muda mfupi ikiwa ni pamoja na kujenga Uwanja wa nyumbani.

Kwa wake Kocha wa Timu hiyo Fredy Felix Minziro amesema, katika kuhakikisha anaboresha kikosi hicho atasajili wachezaji wachache ambao ni wazawa na hana mpango wa kusajili wachezaji wengi au wa Kimataifa na hata kama ikitokea kuhitaji mchezaji wa kimataifa itawalazimu kushauriana na kumuangalia zaidi.

Kocha Minziro amesema, anaamini kikosi kilichoipandisha timu hiyo kwenda Ligi kuu ni kizuri na chenhe uwezo hivyo haoni sababu ya kukifanyia marekebisho makubwa.
Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment