USHINDANI VPL WAWAPA PRESHA RUVU SHOOTING, WAJITABIRIA MAKUBWA MPAKA MWISHONI MWA MSIMU HUU.



Uongozi wa Ruvu Shooting umesema ubunifu wa mbinu mpya za kuboresha kikosi chao unaofanywa na benchi zima la ufundi ndio unaosaidia timu kuwa bora zaidi katika michezo ya Ligi kuu uliombele yao. 


Afisa habari wa Ruvu Shooting Masau Bwire, amesema licha ya mbinu za Makocha lakini wachezaji pia wapo makini katika kuzingatia kile wanachofundishwa ambapo ndiyo sababu  ya jana kuibuka na ushindi dhidi ya Kagera Sugar na ameongeza kuwa kwa sasa hakuna kulala kwani mawazo na akili zote wameelekeza katika mchezo unaofuata. 

"Kila kunapokucha benchi lote la ufundi kwa kushirikiana na makocha huwa wanabuni mbinu mpya za kuiboresha Ruvu Shooting, wanajitahidi kucheza na mapungufu waliyoyaona kupitia mchezo uliopita na hatimaye kuiweka timu katika ubora zaidi kwa lengo la kufanya vizuri katika mchezo unaokuja, " amesema. 

Masau amesema, ushindi dhidi ya Kagera Sugar hauwafanyi kujisahau kwani Ligi ya sasa haiitaji kulala bali wanapaswa kupambana ili kutafuta namna  bora zaidi ya kutafuta matokeo mazuri.

Masau amesema mchezo wanaoutazama kwa sasa ni dhidi ya Lipuli FC mwishoni mwa wiki hii utakaopigwa Uwanja wa Mabatini Mkoani Pwani hivyo wapo katika maandalizi mazuri kutokana na nguvu ya ushindani waliyonayo wapinzani wao. 

"Mechi yetu tunayoitazama kwa sasa ni mechi ya Jumapili hii ambapo tunakwenda kupambana na Lipuli kutoka Iringa katika Uwanja wetu wa nyumbani, wapinzani wetu sio wakubezwa kwani ukiangalia mechi zake zilizopita unaona kabisa hali ya ushindani wanayoionyesha hivyo Kocha anaendelea kukifua kikosi ili kuhakikisha kinafanya vizuri zaidi mwishoni mwa wiki hii, " amesema. 

Katika suala la ushindani uliopo ndani ya Ligi Masau amesema uwiano wa pointi unazidi kumpa mashaka lakini licha ya nafasi waliyopo hajaacha kuitabiria nafasi watakayobaki nayo mpaka hitimisho la msimu huu. 

"Hali ya ushindani kwakweli ni mgumu Sana na sijawahi kuona ushindani ya namna hii kwani hata anayeongoza Ligi hapishani sana na wa chini yake na hata anayeburuza mkia pia hapishani sana na anaofuatana nao, hili linanipa wasiwasi sana lakini naamini tutamaliza Ligi tukiwa katika msimamo mzuri na nimejitabiria mwenyewe kuwa tutamaliza tukiwa si zaidi ya nafasi ya tano Kwenye Ligi, " amesema.


Share on Google Plus

About Tiktak

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment